Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Singida BS Yapigwa Bei, kuanza Kuitwa Singida Fountain Gate FC
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Singida BS Yapigwa Bei, kuanza Kuitwa Singida Fountain Gate FC

    David MohamedBy David MohamedJune 14, 2023No Comments3 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Klabu ya Singida BS imeuza hisa zake kwa mmiliiki wa Fountain Gate huku moja ya masharti ya mkataba ambao wameingia ikiwa ni pamoja na kutobadili jina na maskani ya timu hiyo.

    Viongozi wa taasisi hizo mbili walikutana leo, Jumatano Juni 14 kwenye jijini Dar es Salaam na kuutangazia umma kupitia mkutano na waandishi wa habari juu ya hatua hiyo.

    Aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Singida BS, John Peter alisema katika mkutano huo; “Kwa mwaka mmoja tumekuwa kwenye Ligi Kuu, baada ya kupanda Ligi tulibadili jina na kuitwa Singida Big Stars, malengo yetu yalikuwa ni makubwa, ilikuwa kuingia kwenye nne bora,”

    “Wenzetu wa Tukuyu waliingia Ligi Kuu na kuchukua ubingwa tofauti na sasa ambapo Ligi ni tofauti na zamani, Ligi hii imekuwa na uwekezaji mkubwa, hivyo hata ushindani nao umekuwa mkubwa,”

    “Msimu ujao tutashiriki michuano ya Kimataifa, lazima tujipange na kuona tutafanikiwa kwa namna gani, tumekuwa navikao vingi, kazi kubwa sana imefanyika kufika hapa,”

    “Tunawashukuru wadhamini wote, wametusaidia kuwa hapa, wametusaidia kusafiri bila matatizo na kuweka kambi bila tatizo, tumeshiriki mapinduzi na kushika nafasi ya pili yote haya mafanikio ni kwa sababu ya uwepo wao,”

    Hakuishia hapo aliendelea kwa kusema; “Siku hizi gharama za uendeshaji wa klabu ni kubwa sana, tumetafakari hili pamoja na changamoto tulizonazo, tukatafuta na kuona nani wa kumtua mzigo, tukaona tuungane na hawa ndugu zetu wa Fountain, tulizungunza nao hawa wenzetu ambao wanajua kuhusu mpira kwa sababu wamekuwa na timu ya daraja la kwanza na hata Ligi Kuu kwa upande wa Wanawake,”

    “Tumewasogelea ili kufanya nao biashara ili kuendeleza furaha ya mpira, tumekaa nao mezani na kukubaliana vipengele vya kuchukua timu na kununua, moja na sharti kubwa ni timu kubaki Singida na lazima neno Singida libakie kwenye timu ili kuenzi.”

    Kwa upande wake, aliyekuwa Mkurugenzi wa Akademi ya Fountain Gate, Japhet Makau ambaye kwa sasa ni Rais wa klabu hiyo kwenye muundo mpya, alisema; “Tumeona fursa ambayo imetokea Singida BS, baada ya kuona watafute mtu wa kutake-over,”

    “Singida BS, kwetu tumeona ni sehemu nzuri na kuona kuichukua Singida BS, timu kubaki Singida kwetu hiyo sio changamoto kabisa na Fountain inaweza kuwa Tanzania nzima,” alisema.

    Makau alitangaza kwenye mkutano huo kuanzia sasa timu ya Fountain Gate Princess itafahamika kama Singida Fountain Gate Princess ili kukidhi matakwa ya CAF kushiriki michuano ya Kimataifa msimu ujao.

    Miongoni mwa watu ambao watakuwa sehemu ya Bodi ya watu tisa ya Singida Fountain Gate FC, ni Festo Sanga na Mbunge wa Singida Mjini, Mussa Sima.

    caf fountain gate fountain gate fc ligi kuu bara Singida singida big stars singida fountain gate fc tff
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.