Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Simba SC kuwapeleka MKUDE, KYOMBO Ulaya
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Simba SC kuwapeleka MKUDE, KYOMBO Ulaya

    David MohamedBy David MohamedJune 13, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Katika hatua nyingine, wakati uongozi wa Simba SC ukikuna kichwa kwa Banda na Sawadogo, habari kutokana ndani ya kikosi hicho kinasema kuwa, Simba ipo kwenye mipango ya kuwapeleka Ulaya baadhi ya wachezaji wake ambao hawajapata muda wa kutosha kucheza ili wakacheze huko West Armenia inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza nchini Armenia.

    Simba imefikia maamuzi hayo baada ya kuingia mkataba wa kimahusiano na timu hiyo siku chache zilizopita na uongozi wa West Armenia upo Tanzania na uliukuwa mubashara katika mechi ya mwisho ya ligi iliyozikutanisha Simba na Coastal Union uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam na kuzungumza na baadhi ya Wachezaji.

    Ilielezwa na moja ya watendaji ndani ya Simba kuwa Habib Kyombo, Jonas Mkude, Mohamed Mussa, Nassor Kapama na Jimmyson Mwanuke ndio majina ambayo viongozi wa Armenia wamepewa ili kuwatazama kama watawafaa na baada ya hapo mazungumzo yataanza.

    Hata mechi ya mwisho tulikuwa nao pale uwanjani, wanataka wachezaji watatu hadi wanne kwa kuanzia na majina hayo niliyokutajia ndio wamepewa, hivyo watachagua wao kisha mazungumzo ya mikataba na mambo mengine yataendelea kwani bado wako Dar na wataondoka baada ya kumaliza kila kitu.” alisema mtu huyo.

    Ofisa Mtendaji Mkuu wa Simba SC, Imani Kajula alisema walisaini mkataba wa kimahusiano na West Armenia ambapo miongoni mwa vitu vilivyopo ndani ya mkataba huo ni kubadilisha wachezaji, ujuzi na kuendeleza soka la vijana.

    “Makubaliano baina yetu na wao yana fursa sana kwetu na kwa wachezaji.

    Miongoni mwake ni kutoa fursa kwa wachezaji wetu ambao hawapati muda wa kutosha kucheza kwenye timu kubwa kwenda kucheza huko, lakini pia kushirikiana katika kuendeleza soka la vijana,” alisema Kajula

    Ikumbukwe Mkude, Kyombo, Mwanuke na Mussa ni miongoni mwa wachezaji wa Simba ambao kocha mkuu wa chama hilo, Roberto Oliveira ‘Robertinho’ hajawaweka kwenye mipango yake ya msimu ujao na amependekeza wasajiliwe mafundi wengine kwenye maeneo yao.

    Kwa taarifa zaidi za usajili tufatilie hapa.

    banda habib kyombo jonas mkude nassor kapama robertinho sawadogo simba sc west armenia fc
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.