Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Cristiano Ronaldo athibitisha kwamba ataendelea kuwa na Al Nassr
    Biriani la Ulaya

    Cristiano Ronaldo athibitisha kwamba ataendelea kuwa na Al Nassr

    Brenda UlomiBy Brenda UlomiJune 2, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Nassr's Portuguese forward Cristiano Ronaldo celebrates scoring his team's first goal during the Saudi Pro League football match between Al-Nassr and Al-Raed at the al-Awwal Park Stadium in the Saudi capital Riyadh on April 28, 2023. (Photo by AFP) (Photo by -/AFP via Getty Images)
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Msimu wa kwanza wa Ronaldo nchini Saudi Arabia ulifikia tamati Jumatano iliyopita, ingawa mshambuliaji huyo nyota hakuwepo wakati Al-Nassr iliposhinda Al-Fateh 3-0 na kumaliza nafasi ya pili katika ligi. Alisema Ronaldo “Nina furaha hapa, nataka kuendelea hapa”

    Nyota wa Al Nassr, Cristiano Ronaldo, alithibitisha katika mahojiano na Ligi Kuu ya Saudi Arabia kwamba “ataendelea na timu” msimu ujao.

    “Nadhani ligi ni nzuri sana lakini nadhani bado tuna fursa nyingi za kukua. Nadhani ligi ni nzuri, ni ya ushindani. Tuna timu nzuri sana, tuna wachezaji Waarabu wazuri sana. Miundombinu nadhani wanahitaji kuboresha kidogo zaidi. Waamuzi na mfumo wa VAR. Nadhani wanapaswa kuwa haraka kidogo. Mambo madogo mengine wanahitaji kuboresha. Lakini mimi nipo furaha hapa, nataka kuendelea hapa, na nitaendelea hapa,” alisema alipoulizwa kuhusu uzoefu wake wa kucheza katika ligi hiyo.

    “Na kwa maoni yangu, ikiwa wataendelea kufanya kazi wanayotaka kufanya, basi katika miaka 5 ijayo nadhani Ligi ya Saudi inaweza kuwa ya tano (ligi bora) duniani,” aliongeza.

    Ronaldo akiwa amethibitisha nia yake ya kuendelea nchini Saudi Arabia, akisema yeye na familia yake wanafurahia maisha katika Ghuba, tetesi za usajili bado zinaendelea kuhusu uhamisho wake kwenda moja ya vilabu vikubwa barani Ulaya na inatarajiwa kuendelea kwa kipindi chote cha majira ya joto.

    Msimu wa kwanza wa Ronaldo nchini Saudi Arabia ulifikia tamati Jumatano iliyopita, ingawa mshambuliaji huyo nyota hakuwepo wakati Al-Nassr iliposhinda Al-Fateh 3-0 na kumaliza nafasi ya pili katika ligi.

    Ronaldo, ambaye alijiunga na klabu ya Riyadh mwezi Desemba na kufunga mabao 14 katika mechi 16 za ligi, alipata jeraha la misuli siku nne kabla na akapumzika kabla ya mechi za kufuzu kwa Mashindano ya Ulaya ya Ureno dhidi ya Bosnia-Herzegovina na Iceland mwezi Juni.

    Soma zaidi: Habari zaidi kama hizi hapa 

    AL-Nassr Ronaldo usajli
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.