Ilimchukua msimu mmoja na nusu kuhudumu kwenye kikosi cha vijana cha timu hiyo na baada ya hapo nyota yake ilianza kung’ara akianzia kwenye kikosi cha timu ya vijana na kuibuka mfungaji bora wa michuano hiyo, ni kama ilionekana anaweza na ana kitu licha ya kuwa bado alikuwa akicheza kwenye kikosi cha vijana ila nyota nzuri iling’ara kwake.
Kocha mkuu wa kikosi hicho alimuona na kuamua kumoa nafasi ya kufanya mazoezi na kikosi cha timu ya wakubwa na alipoingia kwenye mfumo basi Kocha mkuu wa kikosi hicho kwa wakati huo aliamua kumpa nafasi ya kuwa sehemu ya mchezo mmoja wa Ligi kuu akitazama akiwa kwenye benchi jambo ambalo kadri muda ulivyokuwa unaenda kijana huyo akapata nafasi ya kuingia kwenye moja ya mchezo wa timu hiyo na kilichobaki ilikuwa ni historia tu kwake na jamii yote.
Kwa sasa kijana huyo amekuwa mchezaji muhimu ndani ya kikosi cha Yanga SC na siyo kwa bahati mbaya bali kwa kile anachoonyesha akiwa na kikoai chake cha Yanga SC kwa misimu miwili sasa na kupelekea kuwaweka benchi wachezaji wa kigeni anaocheza nao nafasi hiyo.
Huyu siyo mwingine ni Clement Mzize kijana ambaye maisha yake ya mpira muda mwingi yalikuwa mkoani Iringa eneo la Semtema, miguu yake ikicheza sana kwenye uwanja wa Kihesa, Kigonzile na Samora pia. Ila kwa sasa kijana huyo miguu yake imekuwa ikicheza viwanja vikibwa ndani ya nje ya Tanzania
Clement Mzize ni kijana ambaye ameonyesha ubora wake kwa muda mfupi licha ya kutopita kwenye misingi bora ya mpira wa miguu ukilinganisha na vijana wengine kama Dickson Job, Israel Mwenda, Kibwana Shomari. Licha ya yote hayo bado ameonyesha ubora jambo ambalo linapelekea kuibua tetesi mbalimbali kuhitajika na baadhi ya vilabu vikubwa ndani ya nje.
Kitendo cha Azam FC kuhitaji huduma ya kijana huyo tena kwa kuweka kiasi kikubwa sana cha pesa mezani ili kupata saini yake ni dhahiri kuwa kwa sasa thamani yake ipo juu na ni wakati wake sasa. Licha ya yote hayo ila kijana huyu amekuwa bora sana akiingia kwenye mifumo mbalimbali ya makocha, kivipi ?.
Wakati wa kocha Nasredine Nabi, alikuwa akitumika zaidi akitokea katikati zaidi na alikuwa akionyesha ubora wa hali ya juu akiungana (aki link) vizuri na viungo wa ushambuliaji kwa kutengeneza magoli na kufunga pia. Ila kwa sasa chini ya Miguel Gamondi amekuwa akitokea katikati ila mara nyingi amekuwa akitumika zaidi kama mshambuliaji ila akitokea pembeni zaidi akitengeneza nafasi na ndiyo sababu ya kuwa mshambuliaji pekee kwenye Ligi aliyetengeneza (Assist) magoli mengi akiwa nazo 5 mbili nyuma ya kinara wa (Assist) Ligi kuu.
Anaweza kuingia kwenye mfumo wa Azam FC? Jibu ni ndiyo kwani namna wanavyocheza Azam FC wamekuwa wakitumia mawinga zaidi na kwa nmana anavyocheza Clement Mzize ni dhahiri ataingia kirahisi sana na hiyo inabebwa na uwezo wake wa kutokea pembeni na katikati pia.
Ni ipi njia bora kwake kubaki Yanga SC au kwenda Azam?. Kwa mujibu wangu sioni shida kwa yeye kwenda Azam FC au kuamua kubaki Yanga SC na sababu ni kuwa vyote ni vilabu vikubwa. Ila kwenye upande mwingine ni angalie upande ambao utampa zaidi mafanikio kwenye uoande wa maokoto nikimaanisha malipo kuanzia usajili hadi mshahara wake kwani maisha ya wacheza mpira ni mafupi mno hivyo ni vyema akaanza kutengeneza njia nzuri sasa.
Kiasi walichoweka Azam FC ni kikubwa sana na kimeonyesha kumpa thamani mchezaji huyo na hiyo ni faraja sana kuona mzawa anapewa thamani kubwa hivyo, ila yote ya yote Azam FC kuna nafasi kubwa kwake yeye kucheza zaidi tena kwenye kikosi kinachoanza.
SOMA ZAIDI: Barua Nzito Ya Shabiki Kwa Viongozi Wa Simba Kuhusu Inonga
